Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa 
maelekezo kwa Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge kuhakikisha kuwa 
Mradi wa Maji wa Ng’apa uliopo mkoani Lindi unakamilika ndani ya miezi 
mine na si vinginevyo.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza
 Mama Salma Kikwete mara baada ya kuwasalimia wananchi waliokusanyika 
karibu na mradi wa Maji wa Ng’apa uliopo Mkoani Lindi. Pia Mama Salma 
Kikwete amemshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kumteua kuwa Mbunge wa Bunge 
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
 jambo na Mbunge mteule Mama Salma Kikwete mara baada ya kuwasalimia 
wananchi waliokusanyika karibu na mradi wa Maji wa Ng’apa uliopo Mkoani 
Lindi.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
 na wananchi wa Ng’apa mara baada ya kutembelea mradi wa Maji wa eneo 
hilo ambao unasuasua kukamilika. Rais Dkt. Magufuli ametoa miezi minne 
kwa Mkandarasi kampuni ya Overseas Infrastructure Alliance Private 
Limited ya India kuhakikisha kuwa inakamilisha ujenzi wa mradi huo na 
sio kuleta visingizio.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
 na Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika 
Ikulu ndogo Mkoani Lindi.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
 mara baada ya kumaliza mazungumzo yake na Bodi ya Wakurugenzi wa Benki 
ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) katika Ikulu ndogo Mkoani Lindi. Wakwanza 
kushoto ni Kiongozi wa Wakurugenzi hao Lekhethe Mmakgoshi kutoka Nchini 
Afrika Kusini na Wakwanza kulia ni Mkurugenzi mwingine wa (AfDB) 
Dkt.Nyamajeje Weggoro ambaye ni Mtanzania.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
 Kiongozi wa Wakurugenzi hao kutoka (AfDB) Lekhethe Mmakgoshi mara baada
 ya kumaliza mazungumzo na Bodi hiyo ya Wakurugenzi.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
 jambo na Mmoja wa Wakurugenzi wa (AfDB) Dkt.Nyamajeje Weggoro mara 
baada ya kumaliza mazungumzo na Bodi yao Ikulu ndogo mkoani Lindi.
Sehemu
 ya Mradi wa Maji wa Ng’apa mkoani Lindi ambao Rais Dkt. Magufuli ametoa
 miezi minne kwa mkandarasi anayejenga mradi huo ili uweze kukamilika 
haraka.
PICHA NA IKULU
 











 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment