Home » » MAMA SALMA KIKWETE KATIKA SHEREHE YA KUMBUKUMBU YA KUTIMIZA MIAKA 37 YA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI LINDI

MAMA SALMA KIKWETE KATIKA SHEREHE YA KUMBUKUMBU YA KUTIMIZA MIAKA 37 YA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI LINDI

.

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi kadi ya CCM kwa mwanachama mpya wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Asha Chadenje aliyehama kutoka Chama Cha Wananchi,CUF wakati wa sherehe za uzinduzi wa sherehe za kutimiza miaka 37 ya chama hicho zilizofanyika kimkoa huko Kiwalala, wilayani Lindi Vijijini tarehe 1.2.2013.
 Furaha ya kadi ya CCM
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mama Salma Kikwete akimpongeza aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Mkoa wa Lindi Bwana Ali Omar Chitanda, ambaye amekihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi. Mama Salma baada ya kumpongeza alimtambulisha kwa wananchi akiwa pamoja na Bi. Asha Chadenje wakati wa sherehe za uzinduzi wa miaka y37 ya CCM mkoani Lindi tarehe 1.2.2014.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Mkoa wa Lindi Ndugu  Ali Mtopa akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ili aweze kuzindua rasmi sherehe za kutimiza miaka 37 ya CCM kwa Mkoa wa Lindi kwenye Kata ya Kiwalala huko Lindi Vijijini tarehe 1.2.2014.
IMG 5076, 5119, 5189  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akihutubia mamia ya wanachama wa CCM na wananchi wa Lindi Vijijini wakati akizindua rasmi sherehe za kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi katika mkoa wa Lindi. Shughuli hiyo ilifanyika katika kata ya Kiwalala iliyoko Lindi Vijijini. Sherehe hiyo ilienda sambamba na kumnadi mgombea wa udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi  katika kata hiyo Bwana Shineni Hamis Zahoro katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 9.2.2014.
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi anayewakilisha Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akimnadi Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kiwalala kupitia CCM, Bwana Shineni Hamis Zahoro wakati wa sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Kiwalala terehe 1.2.2014.
 Baadhi ya wananchi katika sherehe hizo
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA, Mkoa wa Lindi Bwana Ali Omar Chitanda,
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi anayewakilisha Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akimnadi Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kiwalala kupitia CCM, Bwana Shineni Hamis Zahoro wakati wa sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Kiwalala terehe 1.2.2014.
 Mgombea wa Udiwani wa Kata ya Kiwalala kupitia CCM, Bwana Shineni Hamis Zahoro wakati wa sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa katika kijiji cha Kiwalala terehe 1.2.2014.
 Mama Kikwete akimwaga sera za CCM
 Kicheko
 Ngoma ya Tambiko inayochezwa na wananchi wa kabila la wamakonde nayo ilikuwa ni kivutio tosha wakati wa sherehe za uzinduzi wa miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa  kwenye kata ya Kiwalala, Lindi Vijijini tarehe 1.2.2014.

 Ngoma ya Tambiko inayochezwa na wananchi wa kabila la wamakonde nayo ilikuwa ni kivutio tosha wakati wa sherehe za uzinduzi wa miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika kimkoa  kwenye kata ya Kiwalala, Lindi Vijijini tarehe 1.2.2014.
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi ,Mama Salma Kikwete akiteta jambo na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi  Mkoa wa Lindi Dr.Maua Daftari (katikati) huku Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Lindi Vijijini akisikiliza wakati wa uzinduzi rasmi wa kumbukumbu ya kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Lindi zilizofanyika katika Kata ya Kiwalala iliyoko Lindi Vijijini tarehe 1.2.2014.
--------------------------

Mama Kikwete awataka wakazi wa wilaya ya Ruangwa kutunza ardhi yao na siyo kuiuza kwa wageni

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka wakazi wa wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi kuitunza ardhi  nzuri na ya rutuba waliyonayo na kutokubali kuiuza  kwa wageni bali waitumie katika kilimo kwa kufanya hivyo watajipatia chakula cha kutosha na hivyo kuepukana na tabia ya kuomba chakula.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa aliutoa wito huo jana wakati wa kilele za sherehe za kutimiza miaka 37 ya  Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika katika kata ya  Likunja wilayani humo.
Mjumbe huyo wa NEC alisema wilaya hiyo imejaliwa kuwa na ardhi nzuri na rutuba ambayo mazao mengi yanastawi kwa wingi kama wananchi hao watumia ardhi hiyo kulima mazao ya vyakula kwa wingi wataepukana na tatizo  la njaa.
“Ardhi ni mali na ikitunzwa vizuri itawatunza hapo baadaye itumieni kulima mazao ya chakula kama mahindi, mihogo na mtu aone aibu kwenda kuomba chakula kwa jirani kwani hata watoto wenu wakila chakula kizuri na kushiba wataweza kuwa na afya njema na kusoma vizuri wawapo shuleni”, alisema Mama Kikwete.
Akizungumzia kuhusu CCM kutimiza miaka 37 Mjumbe huyo wa NEC aliwataka wakazi wa mkoa wa Lindi kutembea kifua mbele  na kujivuna kwani Serikali ya chama chao imefanya mambo mengi ya maana ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, shule, hospitali na kuboresha hali ya maisha ya wananchi wake ukilinganisha na miaka ya nyuma.
“Leo hii kuna baadhi ya watu wanapita na kusema kuwa Serikali haijafanya jambo la maana kitu ambacho si kweli kwani ukilinganisha  na miaka ya nyuma hivi sasa watoto wetu wanaomaliza darasa la saba wanajiunga na elimu ya Sekondari kwa wingi kwani shule zipo.  
Hivi sasa barabara ni nzuri na ni rahisi kwa mtu kusafiri kutoka  eneo moja hadi lingine tofauti na miaka ya nyuma  pia huduma ya afya imeimarika. Nawaomba  msiwe wanyonge tembeeni kifua mbele na pale mpakapoulizwa jibuni hoja kwani majibu mnayo”, alisema Mama Kikwete.
Mama Kikwete pia aliwataka wananchi hao kutunza amani, upendo na mshikamano  uliopo ili waweze kufika mbali kimaendeleo kwani vitu hivyo wakivipoteza ni sawa na kupoteza lulu waliyonayo.
 Amani ikitoweka hakuna jambo lolote litakalofanyika zaidi ya watu kukimbia huku na kule kunusuru roho zao, nchi zisizo na amani watu hawawezi kukusanyika kwa pamoja na kufanya mambo yao pamoja na demokrasia iliyopo nawashauri mjitahidi kuchagua vitu ambavyo vina maslahi ya Taifa.
Alisema, “Hao wanaowashawishi ninyi mfanye vurugu mbona kwao kuna aman?, ni ukweli kuwa mikoa ya Kusini ilikuwa nyuma kimaendeleo lakini sasa neema imepatikana baada ya kuendelea mnataka kurudi nyuma jitahidini kuwa wazalendo  na kutengeneza mazingira ya kujali kwenu kwa kufanya shughuli za maendeleo angalieni  msiwe chanzo cha matatizo katika maeneo mnayotoka”.
Kwa upande wake Mlezi wa Chama hicho katika mkoa wa Lindi Dk. Maua Daftari aliwapongeza wanachama hao kwa kuweza kutekeleza ilani yao ambayo imeweza kuwasaidia kufika miaka 37 na kusema kuwa wasisikitike na maneno ya kashfa yanayotolewa na wapinzani kwani ndiyo siasa ya vyama vingi ilivyo nao kama vyama vingine wamepata mdomo wa kusemea.
“Serikali iliamua kuanzisha mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 ingawa katika kura zilizopigwa na wananchi  asilimia 80 walikataa na asilimi 20 ya wananchi walikubali lakini ilifanyika hivi ili wananchi wengine waweze wafanye kazi kwa pamoja na Serikali kupitia vyama vyao vya siasa na hii ndiyo demokrasia ya kweli”, alisema Dk. Daftari. 
Naye Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Mzee Ali Mtopa aliwataka wapinzani waache tabia ya kukichafua chama hicho bali wakubali kuwa Serikali imefanya mambo mengi ya maendeleo na siyo kutukana viongozi waliopo madarakani bali kila mtu amwage sera za chama chake na siyo kashfa. 
Wakati huohuo  Katibu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Ruangwa  Saidi  Nng’umbanga  ambaye alialikwa katika sherehe hizo aliipongeza CCM kwa kufikisha miaka 37 na kuwa chama cha Demokrasia kwa kuvishirikisha vyama vingine vya siasa katika mambo mbalimbali.
Nng’umbanga alisema mikusanyiko ya wana Lindi na Mtwara ni ishara kuwa katika mikoa hiyo kuna amani ya kutosha na hakuna uhasama miongoni mwa watu kwani wanakutana katika mambo mbalimbali ikiwemo sherehe, misiba na mikutano ya siasa . 
Jumla ya wanachama waliojiunga katika wiki ya kilele cha sherehe hizo ni 1534 kati ya hao kutoka chama cha upinzani cha CHADEMA ni 29 na Civic United Front (CUF) 21 pia Chama hicho kimefanikiwa kuongeza idadi ya ofisi za kata hadi kufikia 142, matawi 1120 na mashina 11100 lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu na wananchi.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Lindi, Ndugu Ali Mtopa mara tu baada ya kuwasili kwenye Kata ya Likunja iliyoko katika wilaya ya Ruangwa ambako zilifanyika sherehe za miaka 37 ya CCM Kimkoa ambapo Mama Salma alikuwa mgeni rasmi tarehe 2.2.2014.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akielekezwa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Lindi,Ndugu Adeline Gefi sehemu ya kupita ili kupokea maandamano ya wana CCM na wananchi wa mkoa huo wakati wa kilele cha sherehe za miaka 37 ya kuzaliwa chama hicho zilizofanyika katika Kata ya Likunja, wilayani Ruangwa tarehe 2.2.2014. Wa kwanza kulia ni Dr. Maua Daftari, Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Lindi.
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, Mama Salma Kikwete akiwapungia wananchi waliofika kwenye sherehe za kilele za CCM kutimiza miaka 37 zilizofanyika kimkoa katika Kata ya Likunja, wilayani Ruangwa tarehe 2.2.2013
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akipokea maandamano ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi wakati wa sherehe za kilele cha kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi  mkoani humo zilizofanyika katika kata ya Likunja iliyoko katika wilaya ya Ruangwa tarehe 2.2.2014.
 Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akipokea maandamano ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi wakati wa sherehe za kilele cha kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi  mkoani humo zilizofanyika katika kata ya Likunja iliyoko katika wilaya ya Ruangwa tarehe 2.2.2014.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizindua shina la wakereketwa la Jumuia ya Wanawake Tanzania (UWT) katika Kata ya Likunja wakati wa kilele ya sherehe ya miaka 37 ya CCM zilizofanyika katika kata hiyo tarehe 2.2.2014. Mara baada ya kuzindua tawi hilo Mama Salma akapokea shada la maua kutoka kwa mmoja wa viongozi wa UWT wa Kata hiyo na picha ya mwisho ikiwaonyesha akina mama wajumbe wa Tawi hilo wakishangilia baada ya uzinduzi huo.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea zawadi kutoka Bibi Mwanahawa Ali, mjumbe wa UWT wa Kata ya Likunja kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Ruangwa wakati wa kilele cha sherehe za CCM kutimiza miaka 37.
 Ngoma za utamaduni  za makabila mbalimbali ya mkoa wa Lindi zilishamiri katika kilele cha sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika  Mkoani Lindi katika Kata ya Likunja huko wilayani Ruangwa. Hata muziki wa kizazi kipya nao uliporomoshwa katika kilele hicho.  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe hizo
 Ngoma za utamaduni  za makabila mbalimbali ya mkoa wa Lindi zilishamiri katika kilele cha sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika  Mkoani Lindi katika Kata ya Likunja huko wilayani Ruangwa. Hata muziki wa kizazi kipya nao uliporomoshwa katika kilele hicho.  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe hizo
Ngoma za utamaduni  za makabila mbalimbali ya mkoa wa Lindi zilishamiri katika kilele cha sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika  Mkoani Lindi katika Kata ya Likunja huko wilayani Ruangwa. Hata muziki wa kizazi kipya nao uliporomoshwa katika kilele hicho.  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe hizo 
 Ngoma za utamaduni  za makabila mbalimbali ya mkoa wa Lindi zilishamiri katika kilele cha sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika  Mkoani Lindi katika Kata ya Likunja huko wilayani Ruangwa. Hata muziki wa kizazi kipya nao uliporomoshwa katika kilele hicho.  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe hizo
 Ngoma za utamaduni  za makabila mbalimbali ya mkoa wa Lindi zilishamiri katika kilele cha sherehe za miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi zilizofanyika  Mkoani Lindi katika Kata ya Likunja huko wilayani Ruangwa. Hata muziki wa kizazi kipya nao uliporomoshwa katika kilele hicho.  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alikuwa Mgeni Rasmi kwenye sherehe hizo
  Mgeni Rasmi katika sherehe za CCM kutimiza miaka 37 katika Mkoa wa Lindi, Mama Salma Kikwete akikata keki maalum ya sherehe na kuwalisha wana CCM waliozaliwa mwaka 1977, ambapo Chama Cha Mapinduzi kilizaliwa.
 Mmoja wa wana CCM akilishwa keki
 Mgeni Rasmi katika kilele cha sherehe ya kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi, Mkoani Lindi, Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi katika sherehe zilizofanyika katika Kata ya Likunja, wilayani Ruangwa  tarehe 2.2.2014.
 Mgeni Rasmi katika kilele cha sherehe ya kutimiza miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi, Mkoani Lindi, Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi katika sherehe zilizofanyika katika Kata ya Likunja, wilayani Ruangwa  tarehe 2.2.2014.
 Baadhi ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Mama Salma Kikwete wakati wa kilele cha sherehe za kutimiza miaka 37 ya chama hicho zilizofanyika katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa tarehe 2.2.2014.
 Baadhi ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Mama Salma Kikwete wakati wa kilele cha sherehe za kutimiza miaka 37 ya chama hicho zilizofanyika katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa tarehe 2.2.2014.
Baadhi ya wana CCM na wananchi wa Mkoa wa Lindi wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Mama Salma Kikwete wakati wa kilele cha sherehe za kutimiza miaka 37 ya chama hicho zilizofanyika katika kata ya Likunja, wilayani Ruangwa tarehe 2.2.2014. Picha zote na John Lukuwi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa