
NA EMMANUEL MBATILO, LINDIUJENZI wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Ndaki ya Kilimo Kampasi ya Lindi unaoendelea kujengwa Ngongo Manispaa ya Lindi kupitia mradi wa HEET umefikia asilimia 23 ikiwa ni miezi mitatu tangu kuanza kwa ujenzi .Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni katika mradi huo, Naibu Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET) Dkt. Liberato Haule amesema ujenzi huo utakapokamilika kampasi hiyo itakuwa na uwezo wa kuchukua Jumla ya wanachuo 800 kwa wakati mmoja.Amesema Mradi huo unalenga kuleta mageuzi katika elimu ya juu ili kuongeza mchango kwenye uchumi wa Nchi kwa kuboresha mazingira ya kujisomea , kufanya...