MKOA WA LINDI UMEPUNGUZA VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA- DC MWANZIVA

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe: Victoria Mwanziva kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack amewapongeza wataalamu wa afya Mkoa wa Lindi kutoka katika Halmashauri zote sita kwa jitihada za kuhakikisha vifo vya mama na watoto wachanga vinapung...

MAADHIMISHO YA SIKU YA UPANDAJI MITI NGAZI YA WILAYA

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mtama, Mhe. Anderson Msumba, anawahamasisha wananchi wote wa kata ya Namupa;kijiji cha Mnamba na wananchi wote wa Halmashauri ya wilaya ya Mtama kwa ujumla kujitokeza kwa wingi na na kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha siku ya upandaji miti ngazi ya wilaya ambayo yanaadhimishwa leo siku ya tarehe 20/03/20...

UJENZI WA KAMPASI YA UDSM LINDI WASHIKA KASI

NA EMMANUEL MBATILO, LINDIUJENZI wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Ndaki ya Kilimo Kampasi ya Lindi unaoendelea kujengwa Ngongo Manispaa ya Lindi kupitia mradi wa HEET umefikia asilimia 23 ikiwa ni miezi mitatu tangu kuanza kwa ujenzi .Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni katika mradi huo, Naibu Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET) Dkt. Liberato Haule amesema ujenzi huo utakapokamilika kampasi hiyo itakuwa na uwezo wa kuchukua Jumla ya wanachuo 800 kwa wakati mmoja.Amesema Mradi huo unalenga kuleta mageuzi katika elimu ya juu ili kuongeza mchango kwenye uchumi wa Nchi kwa kuboresha mazingira ya kujisomea , kufanya...

SERIKALI YAHIMIZA ULINZI WA MAENEO TENGEFU NA HIFADHI YA BIOANUAI

SERIKALI imewataka wananchi na wadau katika Mikoa ya Lindi na Pwani kuendelea kulinda maeneo tengefu na hifadhi ya bioanuai ili yaendelee kubaki na ubora na viwango vilivyoainishwa kitaifa na kimataifa.Hayo yamesemwa Julai 19, 2024 Wilayani Rufiji Mkoani Pwani na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis wakati alipokuwa akizindua hifadhi hai ya Rufiji- Mafia- Kibiti-Kilwa (RUMAKI).Mhe. Khamis amesema mifumo ikolojia iliyopo katika Hifadhi Hai ni miongoni mwa bioanuai muhimu za Ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki inayohifadhi bioanuai nyingi na za kipekee zinazotambulika kitaifa na kimataifa.”Tunapaswa ...

KILA MMOJA ANA WAJIBU KUSIMAMIA MPANGO JUMUISHI WA HUDUMA ZA AFYA NGAZI YA JAMII-DC NGOMA.

Na. Elimu ya Afya kwa Umma.Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi Mhe. Hassan Ngoma amewataka Viongozi Serikali za Mitaa katika Wilaya hiyo wakiwemo Maafisa Watendaji wa Vikiji na Kata kuhakikisha wanasimamia vyema Mpango Jumuishi wa Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kwani utakuwa na Manufaa makubwa katika Sekta ya Afya.Mhe. Ngoma amebainisha hayo tarehe 17, Julai, 2024 Wilayani Ruangwa katika Kikao cha Kuutambulisha Mpango huo kilichokwenda sambamba na Mafunzo kwa Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Afya, Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji vyote vya Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa."Mpango Jumuishi huu ni mzuri na utaleta matokeo chanya kwenye...

VIJANA RUANGWA WAENDELEA KUJITOKEZA KUWASILISHA MAOMBI YA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII KUPITIA MPANGO JUMUISHI

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Chirangalile kata ya Makanjiro Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi   Mohammed Rashidi Abdallah akitoa maelezo kwa mwombaji nafasi za Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kupitia Mpango Jumuishi Viola Ngonyani Na. Elimu ya Afya kwa Umma.Vijana katika maeneo mbalimbali katika Halmashauri ya Wilaya ya  Ruangwa Mkoani Lindi weendelea kuwasilisha maombi ya kuwania nafasi za Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kupitia Mpango Jumuishi.Akizungumza  Ofisini kwake wakati wa kupokea maombi Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Chirangalile kata ya Makanjiro Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi ...
 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa