Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu
 wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi akizungumza na ugeni kutoka Benki 
ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania wakati walipomtembelea ofisini kwake 
mjini Lindi. 
Kaimu
 Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kulia) akitambulisha 
msafara wake kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi (hayupo 
pichani) wakati walipomtembelea ofisini kwake mjini Lindi. Kushoto ni 
Meneja Mikopo, Bw. Samuel Mshote na  Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa
 TADB, Bw. Augustino Matutu Chacha (katikati).
Mkurugenzi
 wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Matutu Chacha 
(aliyesimama) akiwasilisha mada juu ya fursa za mikopo zinazotolewa na 
Benki ya Kilimo kwa Wadau wa Korosho na Ufuta Mkoa wa Lindi uliofanyika 
katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Wadau wa Korosho na Ufuta Mkoa wa Lindi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
Mkuu
 wa Mkoa wa Lindi, Bw. Godfrey Zambi ameiomba Benki ya Maendeleo ya 
Kilimo Tanzania (TADB) kukopesha wakulima wa mazao ya ufuta na mihogo 
ili waweze kulima kilimo cha kisasa na cha kibiashara hasa kwa wakulima 
wadogo wadogo wa mkoani humo.
Bw.
 Zambi alitoa wito huo wakati wa mkutano wa Wadau wa Korosho na Ufuta 
Mkoa wa Lindi uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa 
Mkoa wa Lindi.
Bw.
 Zambi alisema kuwa mkoa wa Lindi ni mkoa uliojaaliwa katika kuzalisha 
mazao ya ufuta na mihogo lakini changamoto kubwa ni mtaji wa kulima 
kibiashara ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.
“Wakulima
 wa mkoa wa Lindi wapo tayari kushiriki katika kuleta mapinduzi ya 
Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara lakini kwa sasa 
suala la mtaji wa kilimo cha kibiashara ni changamoto kubwa,” alisema 
Bw. Zambi.
Kwa
 upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga 
alisema kuwa Benki ya kilimo ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima wadogo
 wadogo waliokuwa kwenye vikundi ili waweze kukopeshwa.
Bw.
 Assenga aliongeza kuwa Benki ya Kilimo pia ipo tayari kuwekeza kwenye 
miradi ya maendeleo ya Kilimo kwa kuipatia mikopo yenye riba nafuu 
zilizo chini ya viwango vya kibiashara kwenye soko.
“Kwa
 kutambua umuhimu wa wakulima wadogo wadogo nchini TADB imedhamiria na 
kujizatiti kuhakikisha inachangia kwa kiasi kikubwa katika  kuleta 
Mapinduzi yenye tija katika Sekta ya Kilimo nchini kwa kusaidia 
upatikanaji na utoaji wa fedha ikiwa ni pamoja sera nzuri zitakazosaidia
 maendeleo ya kilimo nchini,” alisema.
Naye,
 Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha alisema 
kuwa TADB inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma zisizo za kifedha kwa 
wakulima kama vile kujengewa uwezo juu ya uandaaji wa andiko la miradi 
ya Kilimo, pamoja na upatikanaji wa taarifa za masoko, usimamizi wa 
biashara, mafunzo juu ya miradi ya Kilimo na mbinu za majadiliano ya 
mikataba.
 “Tupo
 tayari kutoa mikopo kwa ajili ya kuwanyanyua wakulima kama ilivyolengwa
 na Serikali kupitia mikopo ya pembejeo kuongeza tija kwenye uzalishaji,
 miundo mbinu ya umwagiliaji na ununuzi wa zana za kilimo,” alisema.
Bw.
 Chacha aliongeza kuwa kwa upande wa mikoa ya kusini Benki ya Kilimo 
imejipanga kueendeleza miundombinu ya umwagiliaji na maghala pamoja na 
uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya korosho na mihogo na kuimarisha 
viwanda vya kubangua mazao ya korosho, na kusindika ufuta, mihogo.
Bw.
 Chacha aliongeza kuwa Benki imejipanga kuwezesha uanzishaji wa mashamba
 mapya na ya kisasa ya mihogo, korosho na ufuta mkoani Lindi.
Chanzo Michuzi Blog 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment